UCHAGUZI KENYA 2017 : UJUE MFUMO MZIMA WA MATOKEO - TANZA MEDIA ONLINE

Wednesday 9 August 2017

UCHAGUZI KENYA 2017 : UJUE MFUMO MZIMA WA MATOKEO

Bw Kenyatta na Bw Odinga


Matokeo ya uchaguzi wa urais nchini Kenya yanaendelea kutangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (IEBC).
Mgombea wa urais anahitaji kushinda asilimia 50 na kura moja ili kutangazwa kuwa mshindi, na pia apate asilimia 25 katika angalau majimbo 24.
Ikiwa hakuna mgombea atakayepata kura nyingi, basi uchaguzi mpya kati ya wagombea wawili wanaoongoza utafanyika kabla ya siku 30 kutoka kura ya kwanza kupigwa kutimia.
Wachanganuzi wameigawana Kenya katika mikoa kanda tano kikabila: Kikuyu na makundi yanayohusiana nao (asilimia 21), Luhya (asilimia 14), Kalenjin (asilimia 13), Kamba (asilimia 10) na Luo (asilimia 10).
Uhuru Kenyatta na naibu wake wanarai jamii zao za Wakikuyu na Wakalenjin, wakati Raila Odinga na naibu wake, Kalonzo Musyoka (kutoka jamii ya Wakamba), wanatarajia kuungwa mkono na jamii za Waluo na Kamba.
Odinga pia anatarajia kupata kura nyingi kutoka jamii ya Waluhya. Musalia Mudavadi, ambaye aliwania urais mwaka wa 2013, na anatoka jamii ya Waluhya ni muhimu kwenye kampeni ya Raila Odinga.
  • Nani ana nafasi ya kushinda uchaguzi mkuu Kenya 2017?
Kura kadhaa za maoni zilionyesha ushindani mkali kati ya Kenyatta na Odinga, na kusababisha watu kuanza kufikiria matukio kadhaa yanayoweza kufuata baada ya matokeo ya kura kutangazwa.

No comments:

Post a Comment