RC Makonda Aongoza Mamia Kumuaga mwili wa Joel Bendera - TANZA MEDIA ONLINE

Saturday 9 December 2017

RC Makonda Aongoza Mamia Kumuaga mwili wa Joel Bendera


MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amewaongoza mamia ya watu waliojitokeza  kumuaga aliyewahi kuwa kocha wa Taifa Stars, Joel Bendera katika Viwanja  vya Hospitali ya Lugalo jijini Dar  ambaye anatarajiwa kuzikwa kesho Korogwe, Tanga.

Bendera  aliyefariki Jumatano wiki hii  katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili aliwahi kushika nyadhifa tofauti serikali ikiwemo ili ya Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Mbunge wa  Korogwe  Mashariki na Mjini na  baadaye kuwa Mkuu wa mkoa wa Morogoro na Manyara

No comments:

Post a Comment