Spika wa Bunge Job Ndugai alisimama
Bungeni Dodoma leo September 5, 2017 baada ya kuapishwa Wabunge wapya wa
CUF na kuwataka Wabunge kuheshimu kanuni za kisheria hasa waliokuwa
wanamtolea maneno ya kebehi.
“Taratibu zote zilifuatwa
kuhusu hawa wabunge kuingia hapa Bungeni na kwa kumalizia niseme kuwa
Spika ana nafasi yake, wapo baadhi ya lile kundi walikuwa wakijinadi
kuwa Spika huyu dhaifu.
“Ilipofika kwenye 18 zangu
nikasema hapa ndio udhaifu wangu utakapoonekana. Kama una akili yapo
maneno ambayo hayana lazima wala umuhimu na mwisho utaumia bure.” – Job Ndugai
No comments:
Post a Comment