MBWANA SAMATTA ASHINDA TUZO YA MCHEZAJI BORA AFRIKA KWA WACHEZAJI WA NDANI NA-KUDEDICATE TUZO HII KWA MZEE SAMATTA, RAIS KIKWETE NA WATANZANIA WOTE” - TANZA MEDIA ONLINE
  • Home

TANZA MEDIA ONLINE

  • AD BANNER
    AD BANNER
    Powered by Blogger.

    Video of the Day

    Portfolio

    Top 10 Articles

    • HATIMAYE IDRIS AFUNGUKA : WEMA SI MJAMZITO TENA
      Leo kupitia akaunti yake Instagram mchumba wa sasa wa mwanadada Wema Sepetu ambaye pia ni mshindi wa Big brother Africa...
    • Serikali yawasilisha bungeni mkataba wa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi
        Serikali imewasilisha Mkataba wa Kimataifa wa Mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi la Afrika Mashariki kati ya Serikali ya Ja...
    • Harmonize feat Sarkodie - DM Chick (Official Music Video)
    • PICHA ZA MAZOEZI YA YANGA KUJIANDAA NA MECHI NA AZAM FC
      Mabeki wa wa timu hiyo Andrew Vicent ‘Dante’, aliyeruka juu na Hajji Mwinyi,wakipokonyana mpira. KIKOSI cha Yanga leo kimeendel...
    • TFF KUIKABIDHI SIMBA NGAO MPYA BADALA YA ILE YENYE MAKOSA
      ...
    • MAN UNITED WATWAA UBINGWA WA LIGI KUU YA VIJANA ENGLAND
      TIMU ya Manchester United imetwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England kwa vijana chini ya umri wa miaka 21 kwa mwaka wa pili mfulu...
    • Utani wa Spika Ndugai kwa Naibu Spika Dr Tulia
    • PICHA ZA MATUKIO YA IKULU WAKATI RAIS JPM AKIMUAPISHA JAJI MKUU
       Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimuapisha Profesa Ibrahim Hamis Juma kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania...
    • ULIMWENGU AZIDI PASUA ANGA NDANI YA TP MAZEMBE
      NYOTA ya Mtanzania Thomas Emmanuel Ulimwengu (pichani kulia) imeendelea k...
    • RC MAKONDA AKABIDHI MSAADA WA PIKIPIKI,COMPUTA NA BAISKELI KWA JESHI LA POLISI
      Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda leo September 8, 2017 amekabidhi Pikipiki za Traffic 10, Computer 100 na Baiskeli za kisasa ...

    Friday, 8 January 2016

    Home Unlabelled MBWANA SAMATTA ASHINDA TUZO YA MCHEZAJI BORA AFRIKA KWA WACHEZAJI WA NDANI NA-KUDEDICATE TUZO HII KWA MZEE SAMATTA, RAIS KIKWETE NA WATANZANIA WOTE”

    MBWANA SAMATTA ASHINDA TUZO YA MCHEZAJI BORA AFRIKA KWA WACHEZAJI WA NDANI NA-KUDEDICATE TUZO HII KWA MZEE SAMATTA, RAIS KIKWETE NA WATANZANIA WOTE”

    Unknown January 08, 2016
    Share This:
    Facebook Twitter Google+ Pinterest Linkedin Whatsapp
     “
    IMG-20160108-WA0031
    Siku ya January 7, 2015 itabaki kuwa siku ya kukumbukwa na Mbwana Ally Samatta kwenye maisha yake yote kufuatia kuandika rekodi mpya barani Afrika na Tanzania baada ya kutangazwa mshindi wa tuzo ya mwanasoka bora wa Afrika kwa wachezaji wa ndani kwenye sherehe za ugawaji tuzo za Glo-Caf Awards zilizofanyika Abuja, Nigeria.
    Shaffihdauda.co.tz imepiga story na Mbwana Samatta muda mfupi baada ya kutangazwa mshindi wa tuzo hiyo, Samatta amei-dedicate tuzo hiyo kwa babayake mzazi pamoja na familia kwa ujumla lakini hakuwasahau watanzania waliokuwa nyuma yake kumwombea na kumtakia kila la kheri ili atwae tuzo hiyo.
    Screen Shot 2016-01-08 at 8.13.02 AM
    Shaffihdauda.co.tz: Hongera sana Samatta kwa kufanikiwa kutwaa tuzo hii na kuipeperusha bendera ya Tanzania, unajisikiaje kuwa mshindi wa tuzo ya mchezaji bora wa Afrika based on Africa?
    Shaffihdauda.co.tz: Nakosa la kusema kwakweli, kwa jinsi watanzania walivyokuwa wameniombea na kwa tuzo hii sijui hata nisemaje ili kuwashukuru au sijui nifanyaje kuwashukuru ili wajue kweli nawapenda na niko nao pamoja kwasababu ya maombi na jinsi walivyokuwa wanaonesha imani hata ambayo mimi mwenyewe sikuwanayo kwenye hii tuzo.
    Lakini pia sidhani kama naweza kumsahau Rais mstaafu aliyepita Mh. Jakaya Mrisho Kikwete kwa inspiration ambayo alinipa siku moja ambayo tulikutana nchini Congo DR aliniambia mambo mengi sana ambayo kwa kiasi kikubwa yalini-motivate. Unajua mtu kama Rais anakuja anakwambia mambo ambayo yanakuhusu moja kwa moja na taifa ni jambo kubwa.
    Screen Shot 2016-01-08 at 8.03.15 AM
    Shaffihdauda.co.tz: Alikwambia maneno gani?
    Mbwana Samatta: Ni mengi tulizungumza lakini moja alituambia mimi na Thomas kwamba, tumeonesha njia tusikubali kubakia Afrika tujitahidi kwenda kucheza Ulaya ili kuonesha njia kwa vipaji vingine ambavyo viko nyumbani. Alisema nyinyi ndio icons wetu, watanzania karibu wote tunawategemea nyinyi kwenye medani ya soka, mjitahidi msituangushe.
    Sidhani kama hata wewe mwenyewe nikikwambia unachukuliaje lakini ni maneno ambayo kwa kiasi kikubwa yalini-push kwa kuona ikiwa Rais anasema hivi, je familia yangu au watu wa karibu  pamoja na sehemu niliyotokea wanachukuliaje hili suala lakini ilinipa morali na kusema kweli inabidi nifanye vizuri. Kweli nashukuru Mungu amenisaidia.
    Screen Shot 2016-01-08 at 11.41.44 AM
    Shaffihdauda.co.tz: Tuzo hii inamaana gani kwenye career yako ya mchezo wa soka?
    Mbwana Samatta: Tuzo hii inamaana sana sana, kiasi cha kwamba ni vigumu kuielezea kwasababu tumeona wachezaji wengi wa kiafrika ambao wako Ulaya wanapata mafanikio mengi Ulaya lakini hawana tuzo kama hii lakini hiki ni kitu ambacho sitakuja kukisahau kwenye maisha yangu. Sijui nikuelezeaje ili uweze kunielewa au watanzania waweze kunielewa lakini kwangu mimi inamaana kubwa sana. Sijawahi yani kujihisi hivi kwenye maisha yangu, sijawahi kuwa katika hali hii.
    Screen Shot 2016-01-08 at 8.00.47 AM
    Shaffihdauda.co.tz: Wakati unakua unaanza kucheza mpira, uliwahi kuwaza siku moja katika maisha yako ingeweza kutokea siku kama ya leo?
    Mbwana Samatta: Kwakweli sikuwahi kufikiria yani kama ipo siku nitashinda tuzo yenye heshima kama hii,yani kwakweli sijui. 
    Shaffihdauda.co.tz: Unahisi nini kimesababisha kitu kama hiki leo kuweza kutokea?
    Mbwana Samatta: Mimi nafikiri ni kujituma kwasababu wakati mwaka unaanza kuna baadhi ya rafiki zangu nilikuwa nawaambia nataka mwaka 2015 uwe mwaka ambao sitoweza kuja kuusahau kwenye maisha yangu. Mungu mkubwa wakati mwaka unaanza ari yangu ya kiufungaji na kiuchezaji ilikuwa chilni lakini kitu ambacho kiliweza kunifanya nirudi kwenye ari ni jitihada. Baada ya kuona kwamba hali si nzuri niliongeza sana jitihada katika mazoezi pamoja na kupangilia muda wangu wa kupumzika.
    Screen Shot 2016-01-08 at 8.01.26 AM
    Shaffihdauda.co.tz: Mbwana wewe ni mshindi umekaa sehemu moja na wachezaji waliofanikiwa sana katika level ya juu. Umekaa na Yaya Toure, Andre Ayew na Pierre-Emerick Aubameyang ambaye ametwaa tuzo ya Mwanasoka bora wa Afrika. Unadhani katika siku zijazo unaweza ukachukua tuzo kama aliyochukua Aubameyang?
    Mbwana Samatta: Baada ya kupata tuzo hii naweza nikasema naweza kuchukua hiyo tuzo na ni kitu ambacho kitaleta historia kuchukua mchezaji bora wa Afriaca based in Africa halafu ukachukua tena mchezaji bora wa Afrika ni kitu ambacho ni vigumu kutokea lakini nafikiri naweza ni jitihada, kuomba Mungu na kuheshimu kazi.
    Screen Shot 2016-01-08 at 8.01.46 AM
    Shaffihdauda.co.tz: Nakumbuka ile medal yako ya ubingwa wa Afrika ulii-dedicate kwa mamayako mzazi ambaye kwa bahati mbaya hatunaye duniani. Tuzo hii ya mchezaji bora Afrika kwa wachezaji wa ndani unai-dedicate kwa nani?
    Mbwana Samatta: Nina ma-group mawili au matatu ya ku-dedicate hii tuzo, kwanza tuzo hii nai-dedicate moja kwa moja kwa babayangu mzee Aly Samatta kwasababu kila siku amekuwa ananiunga mkono katika career yangu na maisha yangu ya soka pamoja na familia kiujumla pili nai-dedicate tuzo hii kwa Mh. Rais mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete kwa maneno yake aliyoniambia na kwa jinsi ambavyo alinipa hamasa.
    Lakini tatu ni ya watanzania wote kwa jinsi walivyoniombea na jinsi ambavyo walikuwa wakipenda na kuhitaji mimi nichukue tuzo hii, kwahiyo nadhani tuzo ni yao.
    Screen Shot 2016-01-08 at 8.03.31 AM
    Shaffihdauda.co.tz: Mwambie maneno matatu kijana wa kitanzania ambaye ana-ndoto za kufikia mafanikio uliyonayo hadi sasa.
    Screen Shot 2016-01-08 at 8.02.55 AM
    Mbwana Samatta: Maneno yangu matatu nayoweza kumwambia kijana wa kitanzania ni haya; Jitume, Heshimu, Utapata.
    Screen Shot 2016-01-08 at 8.01.10 AM
    tangazaji namba moja wa michezo Tanzania.
    chanzo : shafih dauda

    Share This:
    Facebook Twitter Google+ Pinterest Linkedin Whatsapp
    Author Image

    About Unknown
    Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of soratemplates is to provide the best quality blogger templates which are professionally designed and perfectlly seo optimized to deliver best result for your blog.

    By Unknown - January 08, 2016
    Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

    No comments:

    Post a Comment

    Newer Post Home
    Subscribe to: Post Comments (Atom)

    Recent

    Popular

    • HATIMAYE IDRIS AFUNGUKA : WEMA SI MJAMZITO TENA
      Leo kupitia akaunti yake Instagram mchumba wa sasa wa mwanadada Wema Sepetu ambaye pia ni mshindi wa Big brother Africa...
    • Serikali yawasilisha bungeni mkataba wa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi
        Serikali imewasilisha Mkataba wa Kimataifa wa Mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi la Afrika Mashariki kati ya Serikali ya Ja...
    • Harmonize feat Sarkodie - DM Chick (Official Music Video)
      Harmonize feat Sarkodie - DM Chick (Official Music Video)
    • PICHA ZA MAZOEZI YA YANGA KUJIANDAA NA MECHI NA AZAM FC
      Mabeki wa wa timu hiyo Andrew Vicent ‘Dante’, aliyeruka juu na Hajji Mwinyi,wakipokonyana mpira. KIKOSI cha Yanga leo kimeendel...
    • TFF KUIKABIDHI SIMBA NGAO MPYA BADALA YA ILE YENYE MAKOSA
      ...

    Comments

    Archive

    Contact Form

    Name

    Email *

    Message *

    Created By SoraTemplates | Distributed By MyBloggerThemes - Blogger Templates