MANISPAA YA UBUNGO YAIKABIDHI CRDB BANK BILLIONI 1.947 YA MIKOPO YA WANAWAKE NA VIJANA. - TANZA MEDIA ONLINE

Wednesday 18 April 2018

MANISPAA YA UBUNGO YAIKABIDHI CRDB BANK BILLIONI 1.947 YA MIKOPO YA WANAWAKE NA VIJANA.




Leo Tarehe 18 April 2018,Halmashauri Ya Manispaa ya Ubungo,Imeingia Mkataba wa Makabidhiano na Kutoa Huduma ya Mikopo ya Wanawake,Vijana na walemavu na Benki ya CRDB,Kwa Niaba ya Halamshauri.

Mstahiki meya,Boniface Jacob ametiliana Saini ya Mkataba na Benki ya CRDB ambapo  wametiliana saini Ya utoaji wa Huduma hiyo.Fedha za Kuanzia Shughuli hiyo Kiasi cha Shillingi Billioni 1.947 Zitapelekwa Benki ya CRDB kwa ajili ya Ugawaji wa Fedha hizo kwenye Vikundi Mbalimbali vya wanawake(40%) Vijana(40) na walemavu(20)
 
Ambapo kiasi kikubwa Billioni 1.947 kitaifanya Halamshauri Kuvunja Rekodi kwa Kuwa Halmashauri Ya kwanza DSM na Tanzania kuwahi kutoa kiasi kingi cha fedha kwa ajili ya Mikopo ya Vijana,wanawake na kundi Maalum la walemavu
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo,Bw.John Kayombo,ameeeleza kuwa fedha hizo ni sehemu ya asilimia 10,za Mapato ya ndani yaliyokuwa yakitengwa na Halmashauri,Kwa Muda wa Mwaka Mmoja,Pamoja na fedha za Mgawanyo wa Halamshauri kutoka Manispaa ya Kinondoni.
 
Aidha Mstahiki Meya,Boniface Jacob Ameeleza kuwa; Halamashauri Ya Manispaa ya Ubungo imefikia hatua ya  kutiliana Saini na Benki ya CRDB baada ya Kushindanisha Mabenki yote ya Tanzania,na Kuangalia Benki yenye Huduma Nzuri kwa wajasiriamali  wake,itakayo kubali kutoa Riba ndogo kwa Wajasiriamali,Na kukubali kuchangia shughuli za Utoaji Huduma hiyo ya kukagua na kuvisaidia Vikundi vya wakopaji.

Mpaka Leo wakina mama 11,312 na Vijana 1,224 wameshajaza fomu za Maombi ya Mikopo kutoka  Halmashauri,kwa kata zote 14 na Mitaa 91 ,Huku wito ukitolewa kwa vijana baada ya  Idadi Ndogo ya Vijana kujotokea kulinganisha na akina Mama.


MWISHO.
Mstahiki meya Amewashukuru Wataalamu wakiongozwa na Mkurugenzi,wabunge na Madiwani wote,kwa Ushirikiano na Jitihada za Kuibadilisha Manispaa ya Ubungo

IMETOLEWA Na
OFISI YA MSTAHIKI MEYA
MANISPAA YA UBUNGO - 18-04-2018

No comments:

Post a Comment