BAVICHA Watoa Kauli na Maamuzi Mapya Baada ya Patrobas Kuhamia CCM - TANZA MEDIA ONLINE

Saturday 2 December 2017

BAVICHA Watoa Kauli na Maamuzi Mapya Baada ya Patrobas Kuhamia CCM


Patrick Ole Sosopi.
KAMATI
Tendaji ya Baraza la Vijana la Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(Chadema), BAVICHA wamefanya uteuzi wa viongozi wake ngazi ya Taifa ili
kujaza nafasi zilizoachwa wazi kufuatia baadhi ya viongozi wao kukihama
chama hicho na kujiunga Chama Cha Mapinduzi hivi karibuni.
 
Katika
uteuzi huo, Balaza hilo limemteua aliyekuwa Katibu wa Bavicha, Patrick
Ole Sosopi kuwa Mwenyekiti mpya wa BAVICHA, baada aliyekuwa mwenyekiti
wa baraza hilo, Patrobas Katambi kuhamia CCM. Ole Sosopo ataitumikia
nafasi hiyo kwa muda wa mwaka mmoja kabla ya uchaguzi kufanyika mwakani
2018.

 
Aidha,
Bavicha wamemteua Mwalimu John Pambalu kuwa katibu wa Bavicha baada ya
nafasi hiyo kuachwa wazi na Ole Sosopi aliyeteuliwa kuwa mwenyekiti wa
muda.
Kabla ya
maamuzi ya teuzi hizo kufanyika, Baraza la Uongozi la Chama hicho
lilikutana jana na kujadiri mwenendo wa chama hicho, kuweka mikakati na
malengo yao pamoja na kutoa mwelekeo mpya wa chama. Aidha chamahicho
waliojadiri hali ya amani hapa nchini pamoja matokeo ya uchaguzi mdogo
wa madiwani uliofanyika wiki iliyopita ambapo waliambulia kata moja kati
ya 43 zilizofanya uchaguzi na kutoa mapendekezo kwa Bavicha kufanya
uteuzi huo.

No comments:

Post a Comment