TMA watoa utabiri wa hali ya hewa hadi Disemba - TANZA MEDIA ONLINE

Monday 4 September 2017

TMA watoa utabiri wa hali ya hewa hadi Disemba


utabiri wa hali ya hewa
Kushoto ni Mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya hali ya hewa TAnzania, Bi. Agness Kijazi na kulia ni Meneja wa kitengo cha utabiri Bwana Samwel Mdunya.

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa utabiri wa hali ya hewa kwa kipindi cha mwezi Oktoba hadi Disemba mwaka huu ambapo inaonyesha kutakuwa na mvua za wastani katika maeneo mengi hapa nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Agnes Kijazi amesema mvua zinatarajia kuwa za wastani katika maeneo ya mikoa ya Kagera, Mara, Mwanza, Geita, Shinyanga, Dar es salam, Tanga, Pwani, Kilimajaro, Arusha, na Manyara ambapo katika maeneo ya Kazikazini mwa mkoa wa Morogoro na Visiwa vya Unguja, Pemba utabiri wake utatolewa mwanzoni mwa mwezi Oktoba .
utabiri wa hali ya hewa
             Bi Agness Kijazi akifafanua jambo.

Aidha Kijazi amesema, katika Ukanda wa Pwani ya Kazikazini (Dar es salam, Tanga, Pwani na Visiwa vya Uguja na Pemba) na maeneo ya Kaskazini mwa Mkoa wa Morogoro, msimu huu wa mvua unatarajia kuanza wiki ya kwanza hadi ya pili ya mwanzoni mwa mwezi Oktoba na kuisha wiki ya nne ya mwezi Disemba ambapo katika Kanda ya Nyanda za Juu Kaskazini Mashariki (Kilimajaro, Arusha na Manyara) mvua hizo zitaanza wiki 3 ya mwezi Novemba na kuisha wiki ya 4 ya mwezi Decemba mwaka huu.

Kijazi ametoa ushauri kwa sekta mbalimbali ikiwepo sekta ya kilimo ili kuandaa pembejeo mapema kwa ajili ya wakulima na kwa upande wa wakulima wameshauriwa kuandaa mashamba mapema ili kuendana na msimu wa mvua.

No comments:

Post a Comment