droo ya kombe la shirikisho:yanga kuwavaa waangola - TANZA MEDIA ONLINE

Thursday 21 April 2016

droo ya kombe la shirikisho:yanga kuwavaa waangola

Baada ya klabu ya Dar es Salaam Young Africans kuondolewa katika michuano ya klabu Bingwa barani Afrika usiku wa April 20 2016 na klabu ya Al Ahly ya Misri kwa jumla ya goli 2-1, sasa wanajiandaa kurudi kucheza Kombe la shirikisho barani Afrika katika hatua ya 16.
Yanga imepangwa kucheza na klabu ya Grupo Desportivo Sagrada Esperança ya Angola katika hatua ya 16 bora ambapo mechi zitachezwa nyumbani na ugenini na baada ya hapo timu nane zitaingia katika hatua ya makundi ya michuano hiyo ya Kombe la shirikisho barani Afrika, Grupo Desportivo Sagrada Esperança ilianzishwa December 22 1976 .
gfd
Yanga ataanza kucheza nyumbani kati ya Mei 6-8 na mechi za marudiano zitachezwa kati ya Mei 16-18 2016

No comments:

Post a Comment