Taarifa ya kifo chake ilitolewa na Ofisi ya Rais George H W Bush na ilieleza kifo chake kimetokana na matatizo ya kiafya ambapo mara kadhaa mama Bush alilazwa hospitalini na siku ya Jumapili aliamua abakie nyumbani akiwa na familia yake.
Januari mwaka 2017, yeye na mumewe rais mstaafu Bush walilazwa kwa wakati mmoja. Yeye alikuwa akitibiwa kutokana na matatizo ya koo, huku mumewe akitibiwa kwa ugonjwa wa nyumonia.
Mama Bush ni mmoja kati wanawake wawili tu nchini Marekani, kuwahi kuwa mke wa rais na mama wa rais. Abigail Adams alikuwa mke wa John Adams, na mama wa rais John Quincy Adams, rais wa sita wa Marekani.
No comments:
Post a Comment