George Weah azungumza na Waliberia kwa mara ya kwanza tangu ashinde uchaguzi - TANZA MEDIA ONLINE

Monday, 1 January 2018

George Weah azungumza na Waliberia kwa mara ya kwanza tangu ashinde uchaguzi




George Weah amezungumza kwa mara ya kwanza tangu atangazwe Ijumaa kuwa mshindi wa kiti cha Urais nchini Liberia katika uchaguzi wa marudio, amesema ataunda serikali ambayo itajikita katika kuboresha maisha ya watu wa Liberia.
Weah ameahidi kuboresha maisha ya watu wa Liberia amesema ndicho kitakuwa kipaumbele chake  cha kwanza atakapoingia madarakani mwezi Januari.

Katika hatua nyingine, mchezaji huyo wa zamani wa mpira wa miguu, amesema wale wote wanaopenda kuwadanganya watu kwa njia za rushwa hawatakuwa na nafasi katika serikali yake.
Weah amesema utawala wake utajengwa katika misingi ya kitaasisi kama alivyoanzisha Rais Ellen Johnson Sirleaf na amewaita raia wa Liberia walioko nchi za nje warejee kushuhudia maisha mapya na bora.
pia rais George Weah awataka raia wa Liberia walio nje kurudi kuijenga nchi.Rais mteule nchini Liberia, George Weah amewashauri raia wa Liberia wanaoishi nchi za ng’ambo kurudi nyumbani ili kusaidia kuijenga nchi yao.

Nyota wa huyo zamani wa mpira wa miguu ambaye amechaguliwa kuwa Rais, amesema hayo wakati wa mkutano wa kwanza na waandishi wa habari tangu atangazwe mshindi katika uchaguzi wa urais nchini humo.

Amesema ujuzi wa watu wa Liberia walio nchi za kigeni unahitajika kuijenga nchi hiyo.
Aidha, Rais Weah amepongezwa baada ya kusema kuwa ufisadi hautavumiliwa katika utawala wake, ambapo Januari 2018 anaingia madarakani rasmi.

No comments:

Post a Comment