Mahakama imeutaka upande wa Mashtaka kukamilisha upelelezi kesi ya Malinzi - TANZA MEDIA ONLINE

Friday 11 August 2017

Mahakama imeutaka upande wa Mashtaka kukamilisha upelelezi kesi ya Malinzi

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo August 11, 2017 imeutaka upande wa mashtaka kuhakikisha unakamilisha upelelezi wa kesi inayomkabili aliyekuwa Rais wa TFF Jamal Malinzi na wenzake.

Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri ameyasema hayo baada ya Wakili wa Serikali, Nassoro Katuga kudai upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika.

Hata hivyo, Wakili wa utetezi, Nehemiah Nkoko alidai kuwa inaonesha vielelezo vilivyofikishwa Mahakamani upelelezi wa kesi upo tayari lakini upande wa mashitaka unachelewesha.
Kutokana na hatua hiyo, Hakimu Mashauri ameahirisha kesi hiyo hadi August 24, 2017.
 

chanzo : Millard ayo

No comments:

Post a Comment